Pennsylvania
Kutoka Wikipedia
Pennsylvania ni jimbo la kujitawala la Maungano ya Madola ya Amerika au Marekani. Iko katika kaskazini-mashariki ya nchi ikipakana na majimbo ya Ohio, West Virginia, Maryland, Delaware, New Jersey na jimbo la New York. Kona ya kaskazini-magharibi yagusa Ziwa Erie na Kanada iko ng'ambo ya ziwa hili.
Mji mkuu ni Harrisburg lakini mji mkubwa ni Philadelphia.
Jina la jimbo latokana na William Penn aliyepewa hapa ardhi ya kuanzisha makazi kwa ajili ya kundi la kidini cha Maquaker. Jina la jimbo latafsiriwa kama "misitu ya Penn". Ilikuwa moja ya koloni 13 asilia za Uingereza zilizoasi dhidi ya nchi mama baada ya mwaka 1776 na kuanzisha Maungano ya Madola ya Amerika .
Pennsylvania ina wakazi 12,281,054 kwenye eneo la 119,283 km². Zaidi ya nusu huishi katika maeneo ya miji mikubwa Pittsburgh na Philadelphia. Kaskazini ya jimbo ina watu wachache.
Sehemu kubwa ya eneo la jimbo ni milima ya Appalachi. Mito mikubwa ni Monongahela, Allegheny na Ohio.
Majimbo na maeneo ya Marekani |
---|
Majimbo ya Marekani |
Alabama • Alaska • Arizona • Arkansas • California • Colorado • Connecticut • Delaware • Florida • Georgia • Hawaii • Idaho • Illinois • Indiana • Iowa • Kansas • Kentucky • Louisiana • Maine • Maryland • Massachusetts • Michigan • Minnesota • Mississippi • Missouri • Montana • Nebraska • Nevada • New Hampshire • New Jersey • New Mexico • New York • North Carolina • North Dakota • Ohio • Oklahoma • Oregon • Pennsylvania • Rhode Island • South Carolina • South Dakota • Tennessee • Texas • Utah • Vermont • Virginia • Washington • West Virginia • Wisconsin • Wyoming |
Mkoa wa Mji Mkuu |
|
Visiwa vya ng'ambo |
Katika Pasifiki: Samoa ya Marekani • Visiwa vya Mariana ya Kaskazini • Guam • Katika Karibi: Puerto Rico • Visiwa vya Virgin vya Marekani • Visiwa vidogo sana vya Pasifiki: • Kisiwa cha Howland • Kisiwa cha Jarvis • Atolli ya Johnston • Kingman Reef • Atolli ya Midway • Kisiwa cha Baker • Atolli ya Palmyra • Kisiwa cha Wake • Kisiwa kidogo cha Karibi: Kisiwa cha Navassa |