Liberia
Kutoka Wikipedia
|
|||||
Wito la taifa: The love of liberty brought us here (Upendo wa uhuru ulituleta hapa) | |||||
Wimbo wa taifa: All Hail, Liberia, Hail! | |||||
Mji mkuu | Monrovia |
||||
Mji mkubwa kushinda miji mingine yote |
Monrovia | ||||
Lugha rasmi | English | ||||
Serikali
• Raisi
• Makamu wa Raisi |
Republic Ellen Johnson-Sirleaf Joseph Boakai |
||||
Ilianza • Tarehe |
na ACS 26 July 1847 |
||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
96,320 km² (102nd) 13.514% |
||||
Idadi ya watu - July 2005 kadiriwa - Msongamano wa watu |
3,482,211 (127th) 31/km² (140th) |
||||
Fedha | dola ya Liberia (LRD ) |
||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
GMT (UTC) - (UTC) |
||||
Intaneti TLD | .lr | ||||
Kodi ya simu | +231 |
Liberia ni nchi iliyoko Afrika ya Kaskazini. Imepakana na nchi za Ivory Coast, Guinea, na Sierra Leone.
Liberia ni nchi iliyoundwa na makabila mbalimbali ya asili nchini humo na wahamiaji weusi toka Marekani. Wamarekani Weusi hawa walikuwa ni watumwa waliopata uhuru ambao kwa kushirikiana na chama cha American Colonization Society waliunda taifa hili na kutangaza uhuru wa nchi hiyo Julai 26, 1847. Wamarekani Weusi hawa waliichukulia nchi hiyo kama nchi ya ahadi kutokana na asili yao kuwa ni Afrika ambako ndiko mababu zao walikotokea kabla ya kupelekwa utumwani Marekani. Hata hivyo, wahamiaji hawa waliendelea kujitambulisha kama Wamarekani na hawakujenga mahusiano ya karibu na wenyeji.
Alama za taifa hili (bendera, kauli mbiu, na nembo ya taifa) na hata muundo wa serikali vilikuwa vikionyesha mahusiano ya karibu kati ya nchi hizi mbili.
Liberia imekuwa katika vita ya wenyewe kwa wenyewe kati ya mwaka 1989-1996 na 1999-2003. Hivi karibuni imefanya uchaguzi uliofanyika kwa amani na kuweza kumchagua mwanamke wa kwanza kuwa Rais barani Afrika, Ellen Johnson-Sirleaf.
Nchi za Afrika | |
---|---|
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad |Cote d'Ivoire | Djibouti | Eritrea | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesoto | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Uhabeshi | Uswazi | Zambia | Zimbabwe | |
Maeneo ya kiafrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika | |
Ufaransa: Mayotte · Réunion | Hispania: Visiwa vya Kanari · Ceuta · Melilla | Ureno: Visiwa vya Madeira | Uingereza: · Kisiwa cha St. Helena · Kisiwa cha Diego Garcia |