Albrecht Dürer
Kutoka Wikipedia
Albrecht Dürer (21 Mei, 1471 - 6 Aprili, 1528) alikuwa mchoraji na mkata nakhshi Mjerumani. Alifahamika pia kama mtaalamu wa hisabati hasa jiometria. Ahesabiwa kama msanii muhimu zaidi wa zama ya mwamko katika Ulaya ya kaskazini.
Yaliyomo |
[hariri] Mitindo ya kazi
Sehemu kubwa ya kazi za Dürer ni chapisho za picha nakhshi katika ubao au shaba. Alichora pia picha kwa rangi za mafuta na rangi za maji.
[hariri] Maisha
Dürer alizaliwa mjini Nürnberg alipoishi na kufa. Wakati ule Nürnberg ilikuwa mji tajiri wa biashara ya kimataifa. Baba yake alikuwa Mhungaria aliyemfundisha ufundi wa kuchonga dhahabu. Alipokuwa kijana alifanya matembezi ya miaka mitano katika Ujerumani, Uholanzi na Uswisi alipoboresha sanaa yake. Baadaye aliongeza safari ya kwenda Italia alipofanya kazi Venezia na kuona mengi.
1494 alifunga ndoa na Agnes Frey akafungua karakana yake. Kazi mashuhuri ya kwanza ilikuwa mfululizo wa picha nakhshi katika ubao 15 kuhusu ufunuo za Yohane.
Aliendelea kuchora picha nyingi za kidini juu ya hadithi na watu wa Biblia. Lakini alitafutwa pia na matajiri na wakubwa waliotaka picha yao. Kuanzia 1512 aliajiriwa mara nyingi na Kaisari Maximilian I.
[hariri] Picha
Picha ya Mwanaume mbele ya ukuta yenye rangi kibichi (1497) |
Picha ya Oswolt Krel (1499) |
Picha ya mtawala Frederiko wa Saksonia (1500) |
||
Picha ya Jacob Muffel (1526) |
Sungura (1502) |
Sala (1508) |
||
Mwanajeshi, Kifo na Sheitani (1513) |