Sulfuri
Kutoka Wikipedia
Sulfuri (salfa, kibiriti) |
|
---|---|
|
|
Jina la Elementi | Sulfuri (salfa, kibiriti) |
Alama | S |
Namba atomia | 16 |
Mfululizo safu | Simetali |
Uzani atomia | 32.065 |
Kiwango cha kuyeyuka | 388.36 K (115.21 °C) |
Kiwango cha kuchemka | 717.8 K (444.6 °C) |
Asilimia za ganda la dunia | 0.05 % |
Hali maada | imara |
Sulfuri (pia salfa au kibiriti) ni elementi simetali yenye namba atomia 16 kwenye mfumo radidia na uzani atomia 32.065. Alama yake ni S. Kwenye hali sanifu ni imara kuwa fuwele zenye rangi ya njano.
Yaliyomo |
[hariri] Kutokea duniani
Hutokea duniani kama elementi tupu hasa kwenye volkeno lakini zaidi kwenye kampaundi ndani ya madini ya sulfidi. Leo hii inapatikana kutokana na mafuta ya petroli wakati yakisafishwa.
Sulfuri ni elementi ya lazima kwa maada hai na seli zote zatumia sulfuri.
[hariri] Matumizi ya kibiashara
Matumizi yake ya kibiashara ni hasa kwa mbolea wa chumvi, lakini pia katika baruti, viberiti na madawa ya wadudu.
[hariri] Sulfuri - kibiriti
Jina jingine la sulfuri ni "kibiriti" (Kar. كبريت) linalopatikana kwa mfano katika tafsiri za Biblia (k.m. Luka 17,29, Ufunuo 9,17). Matumizi ya neno hili kwa ajili ya "vibiriti" yalijitokeza kwa sababu mwanzoni kichwa cha vijiti kilikuwa na mchanganyiko wa madawa yenye sulfuri au "kibiriti" ndani yake. Hivyo tafsiri nyingine ya "vibiriti" ni "vijiti vyenye sulfuri".
[hariri] Viungo vya Nje
[hariri] Tazama pia
- Mfumo radidia
- Orodha ya elementi
Makala hiyo kuhusu "Sulfuri" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Sulfuri kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |