Nyambizi
Kutoka Wikipedia
Nyambizi (pia: sabmarini) ni meli na mara nyingi manowari inayosafiri chini ya maji.
Kuna pia nyambizi zenye shabaha za kisayansi au kibiashara.
Matumizi ya kivita yalianzishwa hasa na Ujerumani wakati wa vita kuu za dunia.
Tangu miaka ya 1950 kuna nyambizi zinazoendeshwa kwa injini za kinyuklia zenye uwezo wa kuzunguka dunia yote chini ya maji. Mara nyingi hubeba makombora ya kinyuklia.
Makala hiyo kuhusu "Nyambizi" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Nyambizi kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |