Ndege (uanahewa)
Kutoka Wikipedia
Ndege (au eropleni) ni chomboanga kikubwa kinachoweza kuruka wakati kikiwa na watu au bidhaa ndani. Tofauti na puto au ndegeputo au ni nzito kuliko hewa hivyo inahitaji chanzo cha nguvu kwa kupanda na kutembea hewani, kwa kawaida enjini ama injini jeti au injini ya parapela pamoja na mabawa.
Ndege zasafirisha watu na mizigo duniani. Ni njia ya haraka ya usafiri duniani kushinda usafiri kawa barabara, reli au meli. Ndege huhitaji uwanja wa ndege kwa kuruka au kushuka isipokuwa aina za pekee kama helikopta zinaweza kushuka au kuruka karibu kila mahali.
Nchi nyingi zina pia ndege za kijeshi kwa ulinzi.
Kati ya makampuni makubwa yanayotengeneza ndege ni Airbus wa Ulaya na Boeing wa Marekani. Kuna makampuni mengi madogo zaidi katika nchi mbalimbali zinazotengeneza aina za ndege pia.