Zebaki
Kutoka Wikipedia
Zebaki au Hidragiri (hydrargyrum) |
|
---|---|
|
|
Jina la Elementi | Zebaki au Hidragiri (hydrargyrum) |
Alama | Hg |
Namba atomia | 80 |
Mfululizo safu | Metali ya mpito |
Uzani atomia | 200.59 |
Valensi | 2, 8, 18, 32, 18, 2 |
Densiti | 13.534 g/cm³ |
Kiwango cha kuyeyuka | 234.32 K (-38.83 °C) |
Kiwango cha kuchemka | 629.88 K (356.73 °C) |
Asilimia za ganda la dunia | 4*10-5 % |
Hali maada | kiowevu |
Mengineyo | kiowevu kwa hali sanifu |
Zebaki (jina la kisayansi: hidragiri) ni elementi na metali duniani. Kikemia ni elementi ya mpito yenye kifupi cha Hg na namba atomia 80 katika mfumo radidia.
[hariri] Majina
Jina la kawaida "zebaki" lina asili ya Kiarabu زئبق (tamka "zibaq"). Jina la kisayansi latokana na lugha ya Kigiriki kupitia umbo la Kilatini. Ndani yake kuna maneno mawili ya ύδωρ (hidor - maji) na Άργυρος (argiros - fedha) yaani "fedha ya majimaji".
[hariri] Tabia
Zebaki ni elementi ya pekee pamoja na bromi inayoonekana kama kiowevu kwenye hali sanifu yaani mnamo 0 °C na shindikizo la kawaida. Rangi yake ni kifedha-nyeupe.
Ni nzito sana kiasi cha kwamba chuma kinaelea ndani yake. Kwa binadamu ni sumu. Inajiunga na metali kadhaa kama aloi menginevyo haimenyuki kirahisi.
[hariri] Matumizi
Matumizi yake ni katika mitambo na madawa. Yajulikana kama kidole cha kipimajoto kwa sababu zebaki hupanua sambamba na kupanda kwa halijoto.
Aloi zake yatumiwa pia katika tiba ya meno kwa kujaza mashimo.
Halfau ni nyongeza katika taa zinazotakiwa kutoa mwanga mkali au katika beteri.
Makala hiyo kuhusu "Zebaki" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Zebaki kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |