Tokyo
Kutoka Wikipedia
Tokyo ni mji mkuu wa Japani. Takriban watu milioni 12 huishi katika jiji la Tokyo ambao ni 10% wa Wajapani wote. Rundiko la mji lina wakazi milioni 35 ni rundiko kubwa duniani.
Tokyo ni kitovu cha Japani kibiashara, kiuchumi na kisiasa.
Mahali pa jiji ni tambarare la Kanto kando la hori la Tokyo.
[hariri] Historia
Awali Tokyo iliitwa "Edo". Wakati ule Kyoto ilikuwa mji mkuu rasmi na mahali pa Tenno au Kaisari wa Japani. Edo ilikuwa mwanzoni bandari ndogo tu. Ilianza kukua baada ya kuwa makao makuu ya Mashogun waliokuwa viongozi wa kijeshi katika Japani.
Katika karne ya 19 Tenno Meiji alihamisha mji mkuu kwenda Edo iliyoitwa "Tokyo" yaani "mji mkuu wa mashariki". Mji ulikuwa na tayari mwisho wa karne ya 19 ilikuwa mji mkubwa wa pili duniani baada ya London.
Tokyo iliharibiwa na moto katika historia yake pia na matetemekjo ya ardhi na mabomu wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Ilijengwa upya na kukua kuwa jiji kubwa duniani.
Ilikuwa mahali pa michezo ya Olimpiki ya 1964.
Makala hiyo kuhusu "Tokyo" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Tokyo kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |