Kutoka Wikipedia
Habari, Naitwa Said Abdallah Said Salim maarufu kama SideMontero kutoka Dar es Salaam Tanzania. Napenda kuendeleza lugha ya Kiswahili katika Kamusi Elezo hii ya Kiswahili. Karibu tushirikiane.
[hariri] Historia Yangu
Said Abdallah Said Salim ndio jina langu halisi.Ninaishi Kiwalani kwa sasa. Nilizaliwa mwaka 1989 Mei 22 Dubai, U A E. Nimezaliwa nikiwa mtoto wa pili kwa mama na wa tatu kwa baba.
Hata hivyo mimi ni mwanaume wa kwanza kuzaliwa katika familia nzima. Nimesoma elimu ya awali katika shule ya Cresent English school. Elimu ya Msingi nilisoma katika shule ya Msingi Zanaki iliyopo Upanga-Mashariki wilayani Ilala mkoani Dar es Salaam. Sikuchaguliwa chaguo la kwanza ingawa nilifanya vizuri katika mitihani yangu mwaka 2004.
Hivyo kwa shingo upande nikaingia kusoma shule ya mtu binafsi Airwing Secondary School kwa sasa imekuwa High School. Nilisoma nusu mwaka mpaka yalipotoka majibu ya chaguo la pili Mei mwaka 2004, hapo nilijiunga katika shule niliyochaguliwa Jamhuri Secondary School mwaka huo huo. Nilihitimu elimu ya sekondari mwaka 2007 katika mchepuo wa sanaa.
Binafsi ninajishughulisha na dili za hapa na pale. Sina ajira rasmi mpaka sasa. Nimeona ni bora nami nichangie hayo machache niliyo nayo katika hii wikipedia.