Romano Prodi
Kutoka Wikipedia
Romano Prodi (* 28 Agosti 1939 Scandiano (Italia)) ni mwanasiasa na waziri mkuu wa Italia.
Yaliyomo |
[hariri] Profesa wa uchumi
Prodi aliwahi kuwa profesa wa uchumi kwenye Chuo Kikuu cha Bologna kati ya 1971 hadi 1999. 1978 aliitwa na Waziri Mkuu Giulio Andreotti kujiunga na serikali yake kama waziri wa viwanda. Baada ya kuvunjika kwa serikali hiyo mwaka 1979 Prodi alirudi kwenye Chuo Kikuu.
[hariri] Waziri Mkuu mara ya kwanza
1996 alipewa nafasi ya kiongozi wa ushirikiano wa "Uliva" uliounganisha vyama mbalimbali vya kisasa akamshinda Silvio Berlusconi na umoja wake wa kisiasa akawa waziri mkuu. Akajiuzulu 1998 baada ya kuporomoka kwa ushirikiano wa Uliva bungeni.
[hariri] Kiongozi wa Ulaya
1999 akachaguliwa kama mbunge wa Bunge la Ulaya akateuliwa kuwa mwenyekiti au raisi wa Kamati ya Ulaya kwa kipindi cha 1999 hadi 2004. Aliongoza Umoja wa Ulaya katika majadiliano ya kupokea nchi kumi kama wanachama wapya mwaka 2004.
[hariri] Waziri Mkuu awamu wa pili
Baada ya kumaliza kipindi chake akarudi katika siasa ya Italia aliposhinda tena uchaguzi wa bunge la mwaka 2006 dhidi ya Berlusconi. Tangu 17 Mei amekuwa waziri mkuu wa Italia mara ya pili akiongoza ushirikiano wa vyama unaoitwa "Unione" ("umoja")..