Wagikuyu
Kutoka Wikipedia
Wagikuyu (pia: Wakikuyu) ni kabila kubwa nchini Kenya lenye watu milioni 7.5 au asilimia 22 za Wakenya wote. Hukaa hasa katika nyanda za juu za Kenya ya Kati katika mazingira ya Nairobi hadi mlima Kenya.
Wenyewe hujiita Agikûyû; Kikuyu ni tahajia tangu zamani za ukoloni na kuandikwa pamoja na Gikuyu. Lugha yao ni lugha ya Kibantu.
Wagikuyu wanaojulikana zaidi kimataifa ni
- Jomo Kenyatta (Rais wa kwanza wa Kenya)
- Wangari Maathai (mwenye Tuzo ya Nobel ya Amani ya mwaka 2004)
- Ngugi wa Thiong'o (mwandishi anayeishi Marekani)