Savana
Kutoka Wikipedia
Savana ni aina ya sura ya nchi penye manyasi na miti michache. Kiasi cha miti kinategemeana na kiasi cha maji au mvua kinachopatikana.
Tabia kuu ya savana ni uhaba wa maji. Tofauti na jangwa maji yapo ingawa ni kidogo. Kiwango cha kawaida ni kati ya milimita 500 na 1500 kwa mwaka.
Savana ina wanyama wa pekee wanaodumu katika mazingira haya. Wengi ni wala majani halafu kuna wala nyama wanaowinda wala majani.
Makala hiyo kuhusu "Savana" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Savana kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |