Nagib Mahfuz
Kutoka Wikipedia
Nagib Mahfuz (1911 - 2006) (Kiarabu: نجيب محفوظ) ni mwandishi nchini Misri aliyepokea Tuzo ya Nobel mwaka 1988 akiwa mshindi wa pili kutoka Afrika aliyepokea tuzo hiyo.
Mahfuz alizaliwa Desemba 11 1911 katika eneo la Gamaliya mjini Kairo. Baada ya shule ya sekondari alisoma falsafa kwenye chuo kikuu cha Kairo akajiunga na utumishi wa serikali katika wizara ya utamaduni na elimu.
Akiwa mtumishi wa serikali alianza kuandika hadithi fupi. Riwaya zake za kwanza kuanzia mwaka 1939 zilihusu maisha ya Misri ya kale wakati wa Mafarao.
Katika miaka ya 1940 alianza kusimulia habari za Misri ya kisasa. Baada ya "Mtaa wa Midaq" aliendelea na riwaya tatu juu ya maisha ya familia ya Kairo katika vizazi vitatu zilizomleta sifa ya kimataifa.
Riwaya yake ya 1959 "Watoto wa mtaa wetu" ilisababisha umgomvi na wataalamu waislamu waliodai inakashifu imani. Riwaya inatoa mfano wa historia ya binadamu wakiwemo watu wanaofanana na Adamu, Musa, Isa na Mohamad. Kitabu kilitolewa kimilango katika gazeti, lakini upinzani wa wataalamu Waislamu uliwalazimisha wahariri kusimamisha riwaya. Hadi leo haikuchapishwa kwa lugha ya Kiarabu katika nchi ya Misri ingawa inapatikana kwa Kiingereza pia toleo la Kiarabu kutoka Lebanon inapatikana kwa siri.
Mwaka 1989 shehe Mmisri Omar Abdul-Rahman alitamka mbele ya wanahabari ya kwamba heri Mahfuz angeadhibiwa wakati ule. Tamko hili lilisababisha jaribio la Waislamu wakali la kumwua Mahfuz. Hadi leo anaishi chini ya ulinzi wa Polisi.