Konsonanti
Kutoka Wikipedia
Konsonanti ni sauti za lugha ambazo katika Kiswahili zatajwa kwa herufi B, Ch, D, F, G, H, J, K, L, M, N, P, Q, R, S, T, V, W, Y na Z
Kwa sauti hizo hewa haiondoki mdomoni moja kwa moja lakini mwendo wake ni pamoja na sauti za pembeni kwa kutumia shingo, ulimi au meno.
Hii ni tofauti na sauti za vokali kama A, E, I, O na U. Hizi ni sauti tupu ambako hewa huondoka mdomoni bila kikwazo au sauti za pembeni.