Hierapoli
Kutoka Wikipedia
Hierapoli ilikuwa mji wa ustaarabu wa Ugiriki ya Kale katika Asia Ndogo au Uturuki wa leo. Maghofu yako karibu na maji ya moto ya Pamukkale.
Mji ulianzishwa mahali pake kwa sababu ya chemchemi za moto ukakua tangu karne ya tatu KK. Ukaendelea hadi nyakati za vita za misalaba ambako imeshambuliwa na kuharibiwa mara kadhaa. Baada ya uangamizi wakati wa tetemeko la ardhi mwaka 1334 ukaachwa na mahali pake hapakaliwa tena.
Mwandishi wa habari za mianzo ya Biblia Papias wa Hierapoli alikuwa askofu wa mji katika karne ya pili.
Hierapoli pamoja na Pamukkale huhesabiwa kati ya mahali pa urithi wa dunia.