Boda boda
Kutoka Wikipedia
Boda boda (pia: bodaboda) ni neno la kutaja baisikeli inayotumiwa kubeba abiria katika Afrika ya Mashariki au "baisikeli ya teksi". Linaweza kumtaja pia dereva wa baisikeli hii.
Asili yake ni kati ya Wajaluo wa eneo la mpakani kati ya Kenya na Uganda karibu na ziwa Viktoria. Inasemekana asili yake ilikuwa huduma ya kubeba abiria kati ya mipaka ya Kenya na Uganda mjini Busia. Hivyo neno la Kiingereza la "border" = "boda" lilikuwa chanzo cha jina "boda-boda" Lakini huduma imeenea sehemu mbalimbali kama vile pwani la Kenya (Mombasa, Malindi) na pia katika Uganda.
Baisikeli ya kawaida inayotakiwa imara hubadilishwa kwa kuweka kiti kirefu kama pikipiki.
[hariri] Pikipiki badala ya baisikeli
Uganda imeona mabadiliko ambako pikipiki zinachukua nafasi za boda boda katika kazi ya kubeba abiria. Kuna makadirio kuhusu mwaka 2004 ya kuwa watu 200,000 Uganda walikuwa madereva wa boda boda ya baisikeli na 90,000 wa boda boda ya pikipiki.