Kumbukumbu la Sheria (Biblia)
Kutoka Wikipedia
Kumbukumbu la Sheria (pia: Kumbukumbu la Torati) ni kitabu cha tano katika Agano la Kale au Tanakh ya Kiebrania.
[hariri] Majina
Kiasili kimeandikwa kwa lugha ya Kiebrania. Wengine wanakiita Kitabu cha Tano cha Musa kwa vile inafikiriwa kuwa Mose ni mwandishi wa kitabu hicho.
Kwa Kilatini kinaitwa Deuteronomium, maana yake “sheria ya pili”. Chaitwa hivyo kwa sababu ndani yake kuna jumla la torati au sheria zilizotangazwa kwa Wanaisraeli katika vitabu vinavyotangulia.
[hariri] Yaliyomo
Yaliyomo yake ni hasa hotuba tatu za Musa kwa Wanaisraeli kabla ya kifo chake. Mahali ni tambarare ya Moabu na wakati ni mwezi wa 11 katika mwaka wa mwisho wa matembezi ya Wanaisraeli.
- Hotuba ya kwanza (sura 1 hadi 4) yarudia matokeo muhimu ya matembezi ya jangwani ya watu wa Israeli. Inaeleza jinsi ilivyo muhimu kumtii Mungu. Kunya maonyo dhidi ya uasi.
- Hotuba ya pili (sura 5 hadi 26) ni sehemu kuu ya kitabu. Humo kuna marudio ya Amri Kumi, sheria kwa ajili ya maisha katika nchi ya ahadi na sura ya 20 ina sheria kuhusu vita.
- Hotuba ya tatu (sura 27 hadi 30) inajadili yale yatakayofuata kama watu hupuuza maagizo ya Mungu au kuyatekeleza. Mwishoni ahadi kati ya Mungu na wanaisraeli inarudiwa na Yoshua ateuliwa kuwa kiongozi mpya baada ya Musa.
- Milango 32 hadi 34 kuna nyongeza kama vile wimbo la Musa, baraka juu ya makabila ya wanaisraeli na taarifa juu ya kifo cha Musa.
Mwanzo Kutoka Walawi Hesabu Kumbukumbu Yoshua Maamuzi Ruthu Samueli I Samueli II Wafalme I Wafalme II Mambo ya Nyakati I Mambo ya Nyakati II Ezra Nehemia Esta Tobit Yuditi Esta Yobu Zaburi Methali Mhubiri Wimbo Ulio Bora Isaya Yeremia Ezekieli Danieli Hosea Yoeli Amosi Obadia Yona Mika Nahumu Habakuki Sefania Hagai Zekaria Malaki